Sheikh Ibrahim Zakzaky, Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria
ambaye kwa miaka miwili sasa anashikiliwa kinyume cha sheria, kwa mara
ya kwanza jana aliruhusiwa kuzungumza na waandishi wa habari.
Ripoti kutoka Nigeria zinasema kuwa,
Sheikh Zakzaky kwa mara ya kwanza jana Jumamosi alionekana hadharani na
kuruhusiwa kuzungumza na baadhi ya vyombo vya habari.
Picha zilizoenea zinamuonyesha Sheikh
Zakzaky akiwa anazungumza na vyombo vya habari huku akiwa na kifaa cha
kitiba shingoni maarufu kama (Neck supporter). Kifaa hiki huwekewa mtu
aliyejeruhika shingoni. Hata hivyo haijajulikana hasa alikuwa
akizungumza kutokea wapi.
Aidha waandamanaji hao wamesisitiza
kwamba, Sheikh Ibrahim Zakzaky, Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya
Nigeria anashikiliwa kinyume cha sheria na vyombo vya usalama vya nchi
hiyo, hivyo anapaswa kuachiliwa huru mara moja. Vyombo vya usalama mjini
Abuja vilivamia maandamano hayo ya amani na kuwatia mbaroni wanachama
saba wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria.
Itakumbukwa kuwa, Sheikh Ibrahim Zakzaky
alitiwa nguvuni na jeshi la Nigeria mwezi Disemba mwaka 2015 baada ya
kuvamia makazi yake katika mji wa Zaria jimboni Kaduna na kufanya mauaji
ya umati dhidi ya Waislamu. Hata hivyo licha ya mahakama kutoa hukumu
ya kutaka kuachiwa huru mwanazuoni huyo, bado vyombo vya usalama vya
Nigeria vinaendelea kumshikilia katika korokoro isiyojulikana.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment