January 14, 2018

 


Mabalozi wa nchi 54 za Kiafrika katika Umoja wa Mataifa wamelaani matamshi ya kudhalilisha yaliyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu Waafrika
 Mabalozi wa nchi 54 za Kiafrika wametoa taarifa wakilaani matamshi ya kibaguzi na ya kudhalilisha yaliyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya nchi za Kiafrika na Wamarekani wenye asili ya Afrika na kumtaka aombe radhi na afute matamshi yake hayo yenye kudhalilisha. 
Trump Alhamisi iliyopita alizitukana Haiti, El Salvador na baadhi ya nchi  za Kiafrika kuwa ni "shimo la kinyesi" na kutaka kusitishwa kuwapokea wahajiri kutoka nchi hizo. Matamshi hayo ya Trump yamekabiliwa na jibu kali kutoka nchi mbalimbali na jamii ya kimataifa ikiwemo Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa. 

Hii si mara ya kwanza kuona matamshi ya kigabuzi yanayotolewa na rais wa sasa Marekani dhidi ya wahajiri yanazusha mjadala na kupingwa vikali. Tangu Donald Trump ashike hatamu za uongozi, amekuwa akichukua hatua na misimamo ya kibaguzi dhidi ya wahajiri, raia wenye asili ya Afrika na Waislamu, jambo lililosababisha mivutano mikubwa ndani ya jamii ya Marekani na nje ya nchi hiyo. Patrick Gathara mchambuzi mtajika wa masuala ya kisiasa wa Kenya amesema kuhusiana na suala hilo kuwa: Matamshi hayo ya kibaguzi na kijahili ya serikali ya Marekani si jambo jipya.  
Huko nyumba pia Rais Trump alichukua uamuzi uliozusha mjadala mkubwa na kupingwa sana pale alipowapiga marufuku kuingia Marekani raia wa nchi saba za Kiislamu zikiwemo nchi tatu za Kiafrika. Trump anachukua hatua hizo huku viongozi wa Washington wakitoa nara katika nyuga za kimataifa kuwa wanaunga mkono haki za binadamu, kaumu na dini mbalimbali. 
Maandamano dhidi ya Trump mjini Washington 
 
 
 
Trump amechukua hatua kama hii dhidi ya nchi za Kiafrika na kujisahaulisha kwamba hali ya aghalabu ya nchi hizo ikiwa pamoja na umaskini, machafuko ya kisiasa na matatizo ya kiuchumi katika nchi hizo, ni matokeo ya uingiliaji kati wa Washington barani humo kwa miaka kadhaa sasa. Vilevile Trump mbaguzi anasahau au anajisahaulisha kuwa, raia wengi wa nchi za Afrika wanaoishi Marekani kama wahajiri wametoa mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi hiyo. Wahajiri wengi na wale wanaotafuta hifadhi wamelazimika kuhamia Marekani kutokana na siasa za nyuma ya pazia za serikali ya Washington barani Afrika ukiwemo uungaji mkono wake kwa makundi yenye misimamo mikali na ya kigaidi, lengo likiwa ni kuvuruga amani na usalama na kupora maliasili na utajiri wa nchi hizo, suala ambalo hatimaye huzisababishia nchi za bara hilo umaskini na hali isiyoridhisha ya kimaisha. 
Ukweli ni kwamba matamshi ya sasa ya Trump yameibua wasiwasi miongoni mwa viongozi wa nchi za Kiafrika. Matamshi hayo ya kichochezi na kibaguzi yanaweza kusababisha hatari kubwa kwa raia wengi wa nchi za Kiafrika wanaoishi Marekani. Kwa msingi huo matamshi haya ya sasa yameibua wimbi la hasira za viongozi wa Kiafrika kadiri kwamba kitendo cha mabalozi wa nchi 54 za Kiafrika katika Umoja wa Mataifa cha kuonyesha msimamo wazi wa pamoja na kupinga matamshi ya kejeli na kudhalilisha ya Rais wa Marekani kinatajwa kuwa ni cha aina yake.
Katika uwanja huo, Ras Mubarak mbunge wa Ghana anazungumzia suala hilo kwa kusema: Nchi mbalimbali zinapasa kumtumia Trump ujumbe mkali kwamba walimwengu kwa pamoja wanapinga na kupiga vita siasa hizo za chuki, za kuzusha mifarakano na zisizo sahihi. Ingawa majibu makali yaliyotolewa kikanda na kimataifa yamemfanya Trump akane kutumia na lugha hiyo chafu, lakini viongozi wa Kiafrika wakiwa ni wawakilishi wa wananchi wa bara hilo bado wanamtaka Trump awaombe radhi rasmi.  

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE