Viongozi wa vyama ndugu vya CDU/CSU na chama cha SPD wamekamilisha
mkutano wao mjini Berlin wa kuangalia uwezekano wa kuanzisha mazungumzo
juu ya kuunda serikali ya mseto miezi mitatu baada ya kufanyika uchaguzi
mkuu wa Ujerumani. Awali, Kansela Angela Merkel alisema vyama hivyo
bado vinakabiliwa na vizingiti virefu kwenye mazungumzo hayo
vinavyopaswa kuondolewa ili kuweza kufikia makubaliano ya kuunda
serikali ya mseto nchini Ujerumani.
Baada ya mazungumzo ya zaidi
ya usiku kucha, muafaka ilifikiwa baina ya pande hizo. Masuala makuu
yanayojadiliwa na wajumbe wa vyama hivyo wanaokutana kwenye makao makuu
ya chama cha Social Democratic SPD mjini Berlin ni pamoja na uhamiaji,
fedha, afya na masuala ya Umoja wa Ulaya.
Kansela wa Ujerumani Angela Merkel
Kiongozi wa chama cha SPD Martin Schulz
Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier
Mwandishi: Sekione Kitojo / Zainab Aziz
Mhariri: Grace Patricia Kabogo
0 MAONI YAKO:
Post a Comment