February 11, 2018

 
Mwenyekiti wa serikali ya Mta a wa Tupendaneakizungumzia tukio

 
Shehe akizungumza na Mwandishi wa Mtandao huu. 

Hii ni laana! ndivyo unavoweza kusema baada ya kijana mmoja aliyetajwa kwa jina la Dullah mkazi wa Chamwino, kibao cha shule Mkoani hapa anadaiwa kufumaniwa akijaribu kumlawiti baba yake mzazi.

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Jumatatu iliyopita Usiku nyumbani kwa mzee mmoja maarufu (jina linahifadhiwa kwa sababu za kimaadili), anayedaiwa kuwa na umri wa miaka 70.

Habari zinasema kijana huyo anadaiwa kumfanyia unyama huo, baba yake ambaye alipiga yowe kuomba msaada 

Akizungumza na mtandao huu, mzee huyo alisema kijana aliyetaka kumfanyia unyama huo ni mtoto wake wa kumzaa lakini hivi sasa ameathirika kwa ulevi, hivyo kama asingepiga yowe kuomba msaada angeweza kutimiza haja yake ya kumlawiti.

"Huyu mwanangu alipofika hapa nyumbani alianza kunipiga akidai kwanini napika chakula kidogo, ndipo alipojaribu kunivua suruali, nilifanikiwa kumdhibiti asinilawiti" alidai mzee huyo

Andrew John ni mmoja shuhuda wa tukio hilo aliuambia Mtandao huu.
"Huyu mzee ... anaishi chumba kimoja na kulala kitanda kimoja na mwanaye huyo ambaye ni mlevi wa kutupwa
"Leo saa 2  usiku tulisikia mzee  akipiga kelele ndani kuomba msaada, tulidhani wamevamiwa na majambazi, tukakimbia na kukuta mlango umefungwa, tulivunja mlango tulipoingia ndani tukamkuta kijana wake amemkumbatia.

"Mzee huyo alidai kijana wake huyo alitaka kumlawiti nasi tuliposikia hivyo tukamshushia kichapo Dullah, baadae tukamwita  kaka yake  naye kwa hasira alitaka kumkata panga, akatuponyoka na  kutimkia kusiko julikana

Akizungumzia tukio hilo, shehe anayeishi mtaa  huo aliyejitambulisha kwa jina la Kudo Said alisema siku hiyo, alikuwa kwa rafiki yake mmoja ambaye anafanya biashara ya kuuza mabegi ndipo  Dullah alipofika akikimbizwa na watu wachache wakiwa wameshika mawe mkononi.

Alisema, aliwazuia wale watu wasimpige ndipo wakaanza kumueleza kilichotokea kabla ya kumuomba amuombee dua
"Aliniambia yeye anakimbizwa na watu kwa sababu anampenda baba yake.
 Nikamuuliza kivipi, au ni kweli alikuwa anataka kumlawiti baba yake kama wale waliokuwa wana kukimbiza walivyosema, akasema hajamlawiti lakii nimuombee ili asirudie tena  basi mimi nikamuombea na baadae akaondoka zake., alisema shehe huyo.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Tupendane Kata ya Chamwino, Francis  Sentimali  siku ya tukio alikuwa mbali na eneo hilo, lakini alipigiwa simu na kuelezwa  kuwa kumetokea tukio hilo na kwa kuwa alikuwa mbali, alishindwa kupata uhakika wa moja kwa moja.

“Niliporudi nilifika na kuchunguza  lakini sikupata jibu la moja kwa moja maana pia hakuna aliyekuja kulalamika rasmi kwangu alisema mwenyekiti huyo,  Alipoelezwa kwamba anachukua hatua gani kwa matukio kama hayo kutokea katika mtaa wake na kwamba Mwandishi wa habari hizi alishuhudia mlango wa mzee huyu ukivunjwa na watu waliofika kumpiga kijana aliyetaka kumlawiti baba yake huyo Mwenyekiti alifunguka.

Kwanza niwatake watu wasichukue sheria mkononi, jamii yetu pia ibadilike kwa kuacha kufanya matukio mabaya katika jamii yetu. Wazazi tuwalee vizuri watoto wetu.
 
 Na Dunstan Shekidele

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE