May 01, 2018

Picha inayohusiana

Mbunge wa Kigoma Mjini, Mhe. Zitto Kabwe amepingana na maamuzi ya serikali ya kukataa kuongeza mishahara ya wafanyakazi kwa kudai kuwa kuongeza mshahara kila mwaka kwa wafanyakazi ni suala la kisheria na ni la lazima.
Mhe. Zitto ametoa maoni hayo leo Mei 01, 2018 kupitia ukurasa ukurasa wake wa mtandao wa Twitter ambapo amesema serikali ni lazima iongeze mishahara ili wafanyakazi waweze kumudu gharama za maisha ikiwemo mfumuko wa bei.
Kupandisha mishahara ya Wafanyakazi ni suala la kisheria. Kiutaratibu Serikali inapaswa kupandisha mishahara kila mwaka kulingana na mfumuko ya Bei ili kulinda nguvu ya manunuzi ya Mfanyakazi. Vyama vya Wafanyakazi HAVIPASWI kukubali maelezo ya kisiasa.“ameandika Zitto.
Hata hivyo, Zitto amevishauri vyama vya Wafanyakazi nchini kupingana na maamuzi hayo ya serikali “Vyama vya Wafanyakazi havipaswi kukubali maelezo ya kisiasa”.
Kauli ya Mhe. Zitto Kabwe imekuja yakiwa ni masaa machache yamepita baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kutangaza kuwa serikali haitaongeza mishahara ya wafanyakazi kwa mwaka huu.Rais Magufuli amesema hayo leo Mei 01, 2018 katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Iringa.

Related Posts:

  • KUONDOKA KWA WACHEZAJI,YANGA YAWATOA HOFU MASHABIKI WAKE       ongozi wa klabu ya Young Africans unapenda kuwajulisha wanachama wake, wapenzi wa soka na wadau kwa ujumla kuwa taarifa za kuhama kwa wachezai wake Didier Kavumbagu na Frank Do… Read More
  • NEW SONG: DIVA ft BOB JUNIOR - MASHALLAH   Baada ya kufanya poa na nyimbo zake kama piga, simu, kwa raha zako  huu ni wimbo mwingine toka kwa mwana dada Diva Loveness hapa kamshirikisha Bob Junio   Skiliza hapa kisha share na wenzio … Read More
  • DIVA KUTAMBULISHA MASHA ALLAH KESHO     Mtangazaji makeke wa kike hapa bongo, anayefanya kipindi cha Ala za Roho cha clouds Fm Diva loveness love, ambaye pia ni msanii wa bongo fleva, kesho anatarajia kutamburiosha wimbo wake mpya unaoitwa Masha … Read More
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISAIDIE WAFANYA KAZI Kumekuwa na vyama vingi vya wafanyakazi, lakini kero za wafanyakazi bado zinaendelea kuwapo. Kwa mfano kuna vyama vya wafanyakazi vyenye lengo la kutetea walimu, hata hivyo bado walimu wengi wanaendelea kuteseka. Hivi… Read More
  • ADAM MCHOMVU, KUACHIA VIDEO MBILI    Mtangazaji wa kipindi cha XXL na Bongo Fleva ya Clouds Fm, Adam Mchomvu a.k.a Baba Jonni,siku ya juma pili anatarajia kudondosha mzigo wa video za nyimbo zake mbili ndani ya Maisha Club. Licha ya… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE