July 30, 2018

 
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Benki ya KCB wamesaini mkataba wa kudhamini Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu wa 2018/19 wenye thamani ya shilingi Milioni 420.
Udhamini huo unakuja siku chache baada ya wadau wa soka kuhoji juu ya udhami wa ligi hiyo baada ya wadhamini wa kuu kampuni ya simu ya Vodacom kumaliza mkataba wao.
Hata hivyo Shirikisho la soka nchini halijaeleza hatua iliyofikia mpaka sasa na mdhamini mkuu Vodacom baada ya kuelezwa kuwa ipo katika mazungumzo na kampuni hiyo juu ya kuongeza mkataba.
Ligi Kuu Bara msimu wa 2018/19 inatarajia kuanza Agosti 22 ambapo tayari ratiba ya msimu mzima imeshatoka.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE