January 08, 2015

  
 Mtayarishaji wa muziki wa bongo flava nchini Tanzania, Man Walter kutoka Combination Sound amepandisha bei ya kurekodia katika studio zake nakufikia shilingi Milioni Moja kwa wimbo ambapo hiyo ni gharama ya kuanzia.Akiongeana Chanzo kimoja cha habari kwa njia ya simu jana jioni, Man Walter amesema kuwa sasa ni wakati wa kuangalia upande wa pili wa sanaa na sio tu kuwaangalia wasanii wanaofanya muziki bila kuwaangalia wanaoutengeneza muziki huo. Man Walter amesema kuwa kama watayarishaji wa muziki wakiendelea kutoza gharama za awali watabaki kuwa maskini huku wasanii wakineemeka kwa kuwa na kipato kikubwa kitu ambacho si sahihi kwani hawa wote wanatakiwa wapate maendeleo ya karibu sawa kila mtu kwa nafasi yake.Aidha Man Walter amesema kuwa Milioni Moja kwa wimbo ni bei ya kuanzia hivyo inaweza kupanda au kushuka inategemeana na aina ya wimbo kwani atakuwa anatoza kulingana na categories za muziki kwani huwezi kufananisha wimbo wa Ali Kiba na wimbo wowote wa Hip Hop.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE