May 19, 2016

Shirika la ndege la Misri (Egypt Air) limetoa taarifa za kupotea katika rada ndege ya shirika hilo iliyokua ikitokea Paris, Ufaransa ikielekea Cairo, Misri.

_89735812_franceegypt4640516
7 

Eneo ndege ilipopotelea.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa abiria 56, wahudumu wa ndege 7, na wanausalama 3 wamo katika ndege hiyo MS804.
Ndege hiyo aina ya Airbus A320 ilikuwa ikiruka umbali wa futi 37,000 (mita 11,300) ilipotelea ukanda wa Mashariki mwa Mediterranean. Maafisa walisema kuwa ndege hiyo ilipoteza mawasiliano na rada saa 2:45 (00:45GMT) kwa saa za Cairo.
5 
Ndege aina ya Airbus A320 iliyopotea.

Taarifa zinaeleza kuwa ndege hiyo iliondoka katika mji wa Paris 23:09 muda wa huko siku ya Jumatano na ilitarajiwa kufika Mji Mkuu wa Misri 03:00 muda wa huko siku ya Alhamisi.
Harakati za kuitafuta na kuikoa ndege hiyo zinaendelea ili kuhakikisha watu wote wanakuwa salama.

Related Posts:

  • Diamond aburutwa Mahakamani na Hamisa Mobetto Mwanamitindo Hamisa Hassan Mobetto amemfungulia kesi ya madai mzazi mwenzie, Msanii Naseeb Abdul @diamondplatnumzkwa madai ya kushindwa kumuomba radhi pamoja na kutotoa fedha za matunzo ya mtoto wao, Abdul Naseeb Juma.… Read More
  • Huu ndiyo utajiri wa Mwanamuziki AY Msanii wa Bongo Flava, Ambwene Yessaya au maarufu kama A.Y ni moja kati ya wasanii waliopata mafanikio makubwa sana kwenye soko la mziki nchini Tanzania. A.Y ambaye alianza mziki na bado yupo mpaka leo tangu miaka ya 9… Read More
  • Familia ya Lissu waitaka Polisi kushughulikia swala la Lissu   Familia ya mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, aliyejeruhiwa na watu wasiojulikana katika shambulia la kujaribu kumuua, wamelitaka jeshi la polisi kutumia ubalozi wa Tanzania nchini Kenya ili kumpata Dereva wa… Read More
  • Mfalme wa Saudia, ziarani Urusi   Mfalme Salman wa Saudi Arabia amewasili Moscow, ikiwa ni ziara ya kwanza kwa mtawala wa kifalme wa nchi hiyo kutembelea Urusi. Katika ziara yake hiyo, atafanya mazungumzo na mwenyeji wake, Rais Vladmir Putin, ikiw… Read More
  • Penzi la Wolper na Brown chali?   Duniani kuna mambo, Ile couple ya Amber Rose na 21 Savage ya Bongo inayomuhusu muigizaji wa filamu  Jackline Wolper na Brown dezaini kama limekufa hivi. Wawili hao ambao walionekana wakiwa wameshibana kima… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE