June 06, 2015


Swali: Fainali ya UEFA itakuwa historia kubwa kati ya Barcelona au Jeventus. Wewe umewahi kufanikiwa mwaka 2009, unaweza kusema chochote juu ya usiku wa fainali ya UEFA?

TH: Ni ngumu sana kufanikiwa kushinda kombe, inatakiwa kuwa na umoja, uwezo na Imani ndani yenu, pia kuwa na hamu ya kushinda pamoja na kujitolea. Siamini juu ya bahati, chochote unachokifanya vizuri ni kwasababu una uwezo wa kukifanya vizuri. Kuna wakati utapata usaidizi mzuri kati ya wenzako kwenye timu lakini sio swala la bahati.

Swali: Unaionaje Barcelona hii na yenu?

TH: Sipendi kufananisha timu lakini naamini hivi sasa Barcelona wana team nzuri sana.

Swali: Timu  hii ya sasa ya Barcelona  unadhani ina wachezaji wazuri safu ya ushambuliaji?

TH: Nadhani hawa wa sasa hivi wameshinda magoli mengi, lakini ishu sio tu kufunga magoli mengi. Upande wangu ni zaidi ya magoli tu, unaweza kurudi nyuma kwenye historia ukaona wachezaji wazuri zaidi waliofanya vizuri pale mbele. Kinachotakiwa ni kuwa na balance nzuri pale mbele, nadhani hawa wa sasa wanayo hiyo balance.

Swali: Unadhani Juventus inaweza kuzuia mapacha watu pale mbele?

TH: Juventus ipo vizuri sana kuanzia Alvaro Morato, Carlos Tevez na Paul Pogba. Kuna Claudio Marchisio na pia tusimsahau Adrea Pirlo. Pia tunajua jinsi gani Juve walivyowazuri pale nyuma na pia wanaweza kukaa na mpira pia. Lakini kwenye hii fainali hawawezi kukaa na mpira zaidi ya Barcelona japokuwa uwezo wa kuzuia wanao.  Kwangu mimi timu yoyote inayotaka kuzuia Barcelona inabidi wazuie timu nzima na sio mchezaji mmoja.

Swali: Unaamini Juventus wanaweza kubadilisha mawazo ya watu na kuwafunga Messi na wenzake?

TH: Chochote kinaweza kutokea kwenye fainali. Nakumbuka Juve Vs Madrid mwaka 98, kila mtu alijua matokea jinsi yatakavyokua lakini mambo yakawa tofauti. Fainali haitabiliki.

Swali: Unatuwa umekaa kwenye kiti unaangalia mechi kupitia Sky Sports,  je utajiskia wivu kwasababu hauchezi ile mechi?

TH: Nimecheza fainali nakushinda lakini nimecheza na kufungwa pia nikiwa na Arsenal. Lakini ningejiskia vizuri kucheza fainali ya mwaka huu pia.

Related Posts:

  • Tahadhari Kuhusu Makachero FEKI Wa TAKUKURU   Tangu kuanza kwa zoezi la kufuatilia wafanyabiashara wanaoficha sukari kwa agizo la Rais wa Jamhuri ya Tanzania Mh. Dr John Pombe Magufuli, kumekuwa na wimbi la watu wanaojiita “makachero wa TAKUKURU  kuto… Read More
  • New Music: Linah – Imani   Msanii Linah ameachia wimbo mpya unaitwa “Imani” umetaarishwa na Producer Nash Designer ni wimbo ambao unaujumbe mzuri sana sikiliza hapa alafu toa maoni yako. … Read More
  • AY, FA waenda Kortini Kuna uwezekano mkubwa, AY na Mwana FA wamefungua kesi ya masuala ya ukiukwaji wa haki miliki za kazi zao. Mwanasheria maarufu nchini, Alberto Msando amepost picha Instagram akiwa kwenye mahakamu kuu ya Tanzania a… Read More
  • Orodha ya Mataifa fisadi zaidi Afrika Mashariki   Baada ya waziri mkuu wa Uingereza David Cameron kunaswa na kamera akiidunisha Nigeria kuwa mafisadi wakuu kote duniani BBC imeamua kuangazia kwa umakini ikiwa matamshi hayo ni ya kweli. Je Nigeria imeorodhes… Read More
  • Kutoka katika kurasa za Magazeti ya leo Jumatano 11 Mei 2016     Habari za Asubuhi mpenzi msomaji, karibu katika kurasa za magazeti leo hii. makubwa yaliyoandikwa ni haya                       &n… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE