March 22, 2016

                            

Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ilala wamepewa mpaka tarehe 24 Machi mwaka huu wawe wamekwenda kuhakikiwa katika ofisi za utawala za Halmashauri hiyo katika kutekeleza agizo la Mhe.Rais Dkt John Pombe Magufuli la kuhakiki watumishi wote wa umma.

Akizungumza kwa njia ya simu ofisini kwake msemaji wa Halmashauri ya Ilala Bi. Tabu Shahibu amesema tangazo limeshatoka na watumishi wote wanatakiwa kufika kuhakikiwa katika ofisi za utawala ambapo wanatakiwa kwenda na nyaraka mbalimbali muhimu zizohusu ajira zao.

Bi Tabu Shahibu amezitaja nyaraka hizo ambazo mtumishi anatakiwa kuambatanisha wakati wa uhakiki wake kuwa ni vyeti halisi vya taaluma,barua ya kuajiriwa na kudhibitishwa kazini, salary slip na picha ndogo za hivi karibuni.

Zoezi la uhakiki linaendelea vizuri na watumishi wengi wamejitokeza kwa wingi na tunategemea kumaliza zoezi hili March 24 mwaka huu ili kuandaa taarifa rasmi ya kujua watumishi halali na wale watumishi  hewaAlisema Bi Tabu.

Aidha Bi Tabu Shaibu amesema kumekuwa na changamoto ya watumishi wengi kutokuwepo kwenye vituo vya kazi ikiwa wengine wapo masomoni na likizo ila wameshatoa taarifa ya kuwaita ili kufanyiwa uhakiki mara moja ili kuendana na muda uliotolewa na Mhe Rais Magufuli wa siku 15.

Zoezi la uhakiki wa watumishi wa umma katika limekuja mara baada ya uchunguzi uliofanywa katika mikoa ya Singida na Dodoma katika Halmashauri 14 na kugunduwa wafanyakazi hewa 202 wanaolipwa mishahara na hivyo Mhe. Rais Magufuli kutoa agizo la kuhakiki watumishi wote katika Wizara,mikoa,Wilaya,Idara,Taasisi na Wakala za Serikali ndani ya siku 15.

MWISHO

Related Posts:

  • Mwasiti amshtua Babu Tale Ukimya wa msanii wa Bongo Fleva,Mwasiti Almas kwenye muziki umemshtua meneja wa msanii Diamond,Babu Tale. Babu Tale alimzungumzia msanii huyo hivi karibuni alipokuwa akifanya mahojiano kwenye kipindi cha XXL ambapo a… Read More
  • Mbiyo za Urais ndani ya CCM, Mwigulu Nchemba achukua fomu leo      Mbio za kumpata mlithi wa kiti cha urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, zinazidi kushika kasi ndani ya chama cha mapinduzi-CCM baada ya wanachama kuzidi kuongezeka katika harakati za kumpata mgombe… Read More
  • Waziri:Mbeki ndiye aliyetoa fedha kwa FIFA    Thabo Mbeki Waziri wa michezo wa Afrika Kusini , Fikile Mbalula, sasa anasema rais wa zamani wa Afrika kusini Thabo Mbeki ndie aliyeruhusu ulipwaji wa fedha ,dola milioni 10 kwa FIFA , hela ambayo sasa i… Read More
  • Kituo cha tembo yatima chafunguliwa   Srikali ya Tanzania imeanzisha kituo cha kwanza cha tembo yatima mjini Arusha. Kituo hicho kinatarajiwa kuhifadhi watoto wa tembo waliopoteza wazazi wao kutokana na vitendo vya ujangili au sababu nyengine. Hatua … Read More
  • January Makmba kufunguka jumapilu ijayo   Mbunge wa Bumbuli, Tanga na Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, January Makamba nae ni mmoja wa walioingia kwenye headlines kwamba na yeye ameingia kwenye list ya wagombea wa CCM kwenye nafasi ya U… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE