June 18, 2016

MTUNZI:ENEA FAIDY
Ilikuwa ni majira ya saa moja jioni ambapo mkuu wa while ya Mabango alikuwa ofisini kwake akiwa amechanganyikiwa sana kwani hali ya shule hiyo ilizidi kutisha sana hasa baada ya kutokea kwa vifo vya wanafunzi kumi na tano mfululizo ndani ya wiki moja tu. Tena vifo vya ghafla tu.

Mkuu wa shule mama Dayana Mbeshi alikuwa kwenye wakati mgumu sana kubaini chanzo cha tatizo lakini bado hakupata majibu.Mara ghafla mlango wa ofisi ukagongwa, akaingia mwalimu wa malezi wa shule hiyo akiwa na USO wa huzuni sana hali iliyomshtua sana mkuu wa shule

"vipi kulikoni?"
"hali mbaya mkuu.. wanafunzi wawili wamefariki tena bwenini" mwalimu wa malezi alizungumza kwa huzuni iliyochanganyika na hofu.
"what? mmh! sio bure.. kuna kitu hapa..!" alisikika mwalimu Mbeshi huku akiinamisha kichwa chake chini na kukiegemeza kwenye kiganja chake.

******
Wanafunzi wengi walionekana kuwa na hofu sana baada ya vifo visivotarajiwa kuzidi kutokea katika shule yao. Kila MTU aliwaza sana juu ya vifo vile huku kila mmoja akihisi zamu yake IPO karibu. Nyuso za huzuni ndizo zilizotawala kwa wanafunzi wote si wa kike wala wa kiume. Hakuna aliyetamani kulala wala kukaa mbali na kundi la watu kwani hofu iliwajaa mioyoni mwao, hawakuweza hata kusoma.

Lakini hali ilikuwa tofauti sana kwa binti Doreen ambaye alikuwa na wiki tu toka ahamie shuleni hapo. Alionekana kutoogopa chochote wala kuguswa na misiba ya wanafunzi wenzake. Kila Mara alionekana akiwa na furaha, hali hii iliwatisha wanafunzi wenzake na kuwafanya wawe na maswali mengi juu yake.

Doreen alikuwa msichana mrembo, sura yake nyembamba iliyopambwa na macho makubwa legevu, kope ndefu nyeusi tii, pua nyembamba iliyochongoka vyema na midomo mizuri yenye mvuto wa aina yake vilimfanya awe tishio kila kona kwani alikuwa ni mzuri kupindukia lakini Tabia  ilikuwa tofauti na uzuri wake.

Wakati wanafunzi wengine wakiwalilia wenzao Doreen alikuwa amejitenga peke take nyuma ya bweni alilokuwa anakaa na kulikuwa na Giza totoro. Alikuwa uchi wa mnyama huku mikono yake ikiwa imeshikilia vitu fulani huku akitamka maneno ambayo aliyaelewa mwenyewe....  
Itaendelea.......
 

Related Posts:

  • Mr.Blue kuitwa baba Hivi karibuni Ni Baada ya zile story zilizovuma na hatimae Byser mwenyewe kukubali kua anategemea kupata mtoto na mpenzi wake wa zamani sanaaa ambae anajulikana kama Wahda Mohamed....Sasa Nyota njema imeshaanza kuonekana ambapo mw… Read More
  • JOBFIRE A.K.A (SAUTI ZA MATUKIO) ASAKA MDHAMINIPICHANI NI MSANII WA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA ANAYEJULIKANA KWA JINA LA JOBFIRE A.K.A SAUTI ZA MATUKIO,, NI MZALIWA WA MOSHI MKOANI KILIMANJARO ILA KAZI ZAKE KIMUZIKI ANAFANYIA KISIWANI ZANZIBAR, CHIMBUKO LAKE NI MKOA WA TANGA,… Read More
  • SELE CHID BEENZ BIFU ZITO    Msanii Afande Sele aligeuka mbogo baada kumjibu msanii mwenzake Chid beenz kuwa hawezi kumteka na hana uwezo huo kwani Afande ameshakua mwanajeshi JWTZ na akaacha jeshi hivyo awezi kutishiwa amani n… Read More
  • KUNDI LA BLUE 3 KURUDI TENA UPYAA..!! Ex Blu3 star who is now rumoured to be back to the group after they reunited with Jackie and Lillian has shown the other side of her by coming to the rescue of a one year old who was burnt by her father after a simple… Read More
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - TAMASHA LA MICHEZO TAMASHA LA MICHEZO LILILOANDALIWA NA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO KWA KUSHIRIKIANA NA UBALOZI WA SERIKALI YA UINGEREZA NCHINI KUPITIA SHIRIKA LA ‘BRITISH COUNCIL’ TAREHE: 27, MACHI, 2012MUDA: 4 Asb- 7… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE