January 21, 2018

Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo Bara, Msafiri Mtemelwa

 Wakati zikiwa zimepita siku tatu tangu CHADEMA watangaze kuwa watashiriki uchaguzi mdogo wa ubunge wa jimbo la Kinondoni na Siha leo Chama cha ACT-Wazalendo kimeendelea kushikiria msimamo wao wa kutoshiriki kwenye uchaguzi huo kwa kuwa sababu zilizowafanya wasusie uchaguzi mdogo uliopita, bado hazijafanyiwa kazi.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jumapili Januari 21, 2018. Naibu Katibu Mkuu waATC Wazalendo Bara, Msafiri Mtemelwa amesema changamoto walizolalamikia katika uchaguzi mdogo uliofanyika Januari 13 katika majimbo ya Songea Mjini, Longido na Singida Kaskazini bado hazijafanyiwa kazi.
Mtemelwa amesema bado chama hicho kitaendelea kushinikiza Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kufanya mageuzi katika mchakato wa uchaguzi.
ACT Wazalendo walilalamikia kuwa kuna matumizi ya nguvu ya vyombo vya dola dhidi ya vyama vya upinzani kwa lengo la kukisaidia chama tawala CCM.
Majimbo ya Siha na Kindondoni yalikuwa wazi baada ya waliokuwa wabunge wa majimbo hayo kuhamia CCM mwishoni mwa mwaka jana.

Related Posts:

  • NDOTO 7 ZA SHEKH SHARIF KUHUSU 2015 ZA WASHTUA WENGI Sheikh Shariff Matongo  akizungumza leo na waandishi wa habari ofisini kwake  jijini Dar es Salaam(hawapo pichani)kuhusu  ndoto yake ambayo ameoteshwa kuelekea mwaka 2015. Sheikh Sharif Matongo amesema … Read More
  • SHOW YA DIMOND RWANDA NI SHEEDDAHH   Usiku wa mkesha wa mwaka mpya Diamond Platnumz amefanya yake katika Vibe Party huko jijini Kigali, Rwanda akiambatana na mpenzi wake mpya Zarinah aka thebosslady kutoka Uganda pamoja na timu nzima ya wasafi na m… Read More
  • UNDANI WA MAHABUSU ALIYEUAWA LEO KISUTU JESHI la Magereza limefanikiwa kumdhibiti Mahabusu  wa Kesi ya dawa za kulevya ambaye ni Raia wa Sieralioni,  Abdul Koroma (33) asitoroke chini ya Ulinzi wa Askari Magereza ndani  Mahakama ya Hakimu … Read More
  • MTOTO WA MIAKA MINNE ATEKWA Kamanda wa polisi mkoani Mwanza Valentino Mlowola Nchini Tanzania katika Kijiji cha Ndami, tarafa ya Mwamashimba wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza watu wasiofahamika wamevunja ny… Read More
  • MVUA KUBWA YANYESHA NA KULETA ATHARI MOROGORO   Gari ya TANAPA ilivyozama leo hii baada ya mvua kubwa kunyesha mkoani Morogoro  Leo hii mkoani Morogoro mvua kubwa ilinyesha na kuleta athari ya uharibifu wa mali mbalimbali,  Mvua hiyo iliyonyesha kwa … Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE