Diva The Bawse ambaye ametoa wimbo wake mpya ‘Mashallah’ siku chache
zilizopita, amesema anajiandaa kuufanyia video pamoja na kuanza tour ya
kuutangaza wimbo huo.
“Video tunatarajia kufanya na aliyefanya ‘Asante’ ya Ay,” Diva ameiambia amesema.
Ameongeza kuwa kwasasa ameamua kuingia kwenye muziki kwa miguu yote
miwili, ndio sababu anatarajia kuanza kufanya tour mikoani kuutangaza
wimbo wake.
“Nahitaji kutumia muda mwingi kuutangaza huu wimbo, ambao uko chini
ya management ya Sharobaro Recs, na ningependa kuulizwa maswali
yanayohusu muziki zaidi kuliko mambo binafsi, nahitaji kuwa na privacy
na ku-focus na biashara yangu, maisha yangu ya radio na muziki.”
Diva ameongeza,
“Pia nina meneja mpya anaitwa Kerry Kerwin ambaye anamsimamia Victoria Kimani akiwa hapa Tanzania, na pia niko tayari kuanza kufanya shows za mikoani. Tutahakikisha huu wimbo unafika katika radio zote za mikoani Tanzania na nje, na habari njema ni kuwa ‘Mashallah’ imeanza kupigwa Nairobi.”
“Pia nina meneja mpya anaitwa Kerry Kerwin ambaye anamsimamia Victoria Kimani akiwa hapa Tanzania, na pia niko tayari kuanza kufanya shows za mikoani. Tutahakikisha huu wimbo unafika katika radio zote za mikoani Tanzania na nje, na habari njema ni kuwa ‘Mashallah’ imeanza kupigwa Nairobi.”
0 MAONI YAKO:
Post a Comment