February 26, 2015

 
Bwana huyo ambaye taswira yake akiwachinja mateka kwa kisu bila huruma ndiyo nembo ya wapiganaji hao sasa ametambuliwa kuwa anatokea Uingereza.
Shirika la Habari la BBC limetambua kuwa jina lake kamili ni Mohammed Emwazi.
Emnuazi ameonekana kwenye video kadhaa ya mauwaji ya mateka wa mataifa wa magharibi, akiwemo Mmarekani James Foley, Raia wa Uingereza, Alan Henning na mwaandishi habari wa Japan, Kenji Goto.
Inaaminika kuwa Emwazi ni raia wa Uingereza na hasa anatokea magharibi mwa London.
Yamkini Emnuazi aliyezaliwa Kuwaiti na mwenye umri wa kati ya miaka 20 -29 alikuwa amefahamika sana na vyombo vya usalama lakini kwa sababu za kiusalama haikuwezekana kumtambua.
Anaaminika amewahi kuishi Somalia mnamo mwaka 2006 na anauhusiano mkubwa na kundi la wapiganaji wa Al Shabab nchini humo.
Polisi nchini Uingereza imeziomba vyombo vya habari kutosambaza habari ambazo hawajazithibitisha kumhusu jamaa huyo kwani uchunguzi unaendelea.
Hata hivyo bado habari za kina kumhusu Jihadi John hazijatolewa.
Mwandishi wa maswala ya Usalama wa BBC Tomi Oladipo anasema kuwa vyombo vya usalama vya serikali za mataifa yanayokaribia Somalia sasa yana kila sababu ya kutahamaki.
Bwana huyo aliwahi kushirikiana na kundi la Al Shaabab
 

Kwa sababu Kuhusika kwake na kundi la Al Shaabab kisha akajiunga na kundi la Islamic State ambalo kwa wakati mmoja lilikuwa linashindana na wanamgambo wa Al Qaeda kuhusu yupi kati yao anayeushawishi
mkubwa
Ishara kuwa Al Shabab inazingatia msimamo mkali wa kidni hata zaidi ya Al Qaeda.
Kwa sababu itakumbukwa kuwa Al Qaeda ilipinga hatua kali ya kuwachinja mateka nchini Iraq na Syria.
Emnuazi ambaye amekuwa akiwabeza mataifa ya Magharibi kabla ya kuwakata shingo naaminika kuwa mtaalamu wa maswala ya kompyuta alisomea chuo kikuu cha Westminster.
Kwa mujibu wa mwandishi wa BBC bwana huyo anaaminika kuwa alikwenda Syria mwaka wa 2012, lakini kabla ya wakati huo majasusi wa Uingereza na Marekani walikuwa hawajajua tishio lake.

Related Posts:

  • Ngassa ajutia nafasi, ailalamikia Yanga   Na Richard Bakana, Dar es salaam MSHAMBULIAJI wa klabu ya Yanga na Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mrisho Ngassa, amejutia uamuzi wake wa kukataa kujiunga na El Merreikh ya Sudan akisema kuwa yalikuwa ni… Read More
  • UN yailaumu Tanzania kwa hali ilivyo DRC   Umoja wa mataifa imezituhumu serikali za Tanzania na Burundi kuhusiana na hali katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Ripoti mpya ya kundi la wataalamu wa umoja huo kuhusu Congo, imeituhumu Tanzania kwa kuwaruhu… Read More
  • Mbasha asita kuzungumzia mtoto wa mkewe    Mwimbaji wa miondoko ya injili nchini, Emmanuel Mbasha hatimaye amefunguka juu ya mtoto ambaye mkewe Flora Mbasha amejifungua na kuweka wazi kuwa, kwa sasa asingependa kusema chochote juu yake mpaka pale wa… Read More
  • Cindy Sanyu amponda Miss Uganda live   Msanii wa muziki kutoka nchini Uganda, Cindy Sanyu ameibua mjadala mzito mtandaoni baada ya kufunguka wazi kuwa mrembo anayeshikilia taji la miss Uganda kwa sasa, Leah Kalanguka ana muonekano mbaya, na kukazia … Read More
  • Ruby ameamua sasa kuuachia wimbo wake rasmi mtandaoni. Pakua hapa   Ni msanii chipukizi kabisa katika anga ya muziki wa Bongo fleva, wimbo wake huu ndiyo wa kwanza lakini umeonekana kuteka hisia za watu wengi sana kwa sasa, anaitwa Ruby wimbo unaitwa na yule. Tenga muda wa kuuskia n… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE