Lakini tumeongea na uongozi wake kutaka kujua nini sababu za kuchelewa kutoka kwa video hiyo, na umesema kuwa kuna vitu vichache vimechelewesha na kwamba mashabiki wasiwe na shaka kwasababu kiu yao itakatwa.
“Kuna vitu vinachelewesha ila tupo katika final touches,” meneja wa Diamond, Sallam ameiambia Bongo5.
“Ukiwapa kitu kibaya watalalamika ni bora wafanye subira wapate kizuri zaidi,” ameongeza.

Ijumaa hii Diamond alipost kwenye Instagram picha ya mwanae Tiffah mwenye umri wa miezi 11 sasa na kuandika: On the LONG conversation with my Miss World before Making a History.”
Ujumbe huo uliwapa matumaini mashabiki wake kuwa muda wa kuiona video hiyo umekaribia.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment